WATAKIWA KUACHA KUPUUZA SERA YA WAZEE

HALMASHAURI  na Vituo vya afya mbalimbali nchini zimetakiwa kuacha kupuuza sera ya wazee na badala yake kuhakikisha kuwa wanafuta sera hiyo vema kwa kuwa baadhi ya wazee hapa nchini wanakabiliwa na changamoto lukuki ikiwemo changamoto ya uhaba wa kipato

Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa na mwenyekiti wa chama cha wazee (CHAWAMA) bw Eliniradhi Msuya wakati akiongea na wazee mbalimbali wa jiji la Arusha mapema wiki hii.

  Msuya alifafanua kuwa mtabia hiyo ya kuwakwepa wazee inaendelea kuzaa matunda makubwa sana hapa nchini kwa kuwa baadhi yao wanaonekana kama kero hasa katika vituo vya afya

Aliongeza kuwa  wazee kama wazee wanakabiliwa na changamoto lukuki hivyo ni jukumu la wahusika kuhakikisha kuwa wanatekeleza sera mbalimbali za wazeee na wala sio kuwapuuza kwa kuwa wana haki kwa mujibu wa sera yao

Pia alisema kuwa hata katika halmashauri nazo zinatakiwa kuhakikisha kuwa zinakuwa na mafungu maalumu kwa ajili ya kuweza kuwasaidia wazee ambao wengine ni walezi huku umri wao ukiwa umekwenda sana

Alieleza kuwa endapo kama wazee watatengewa bajeti yao itakuwa ni raisi sana kuweza kubaini matatizo mbalimbali ambayo wanakabiliana nayo hata kwa kupitia kwa chama hicho tofauti na sasa ambapo halmashauri nyingi sana zinawakwepa wazee .

Awali mwenyekiti huyo aliwataka wadau wa elimu nao kuweza kuwaangalia zaidi wazee hasa wale wa vijijini kwa kuwa baadhi yao wanakabiliwa na changamoto ya kubwa sana ya kulea wajukuu huku wakiwa hawana kipato cha uhakika,lakini kama wadau hao wakijitokeza kwa wingi na kisha kuwasaidia zoezi hilo la kuwalea wajukuu basi watakuwa wamesaidia kwa kiwango cha hali ya juu sana upatikanaji mzuri wa sera ya wazee hapa nchini.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia