KARIBU TENA TANZANIA


RAIS wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed akiagana na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete hivi leo katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa kilimanjaro 
 
RAIS wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed  ameushukuru uongozi wa serekali ya Tanzania kwa jinsi wanavyoendelea kutoa misaada mbalimbali katika nchi yao.
 
 
Hayo aliyasema  jana (leo) wakati alipokuwaakimaliza ziara yake ya siku tatu hapa nchini iliyokua na lengo la kuomba misaada mbalimbali ya kibinadamu kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete na serikali ya Tanzania.
 
Alisema kuwa serekali ya Tanzania imekuwa ikiwasaidia katika vitu mbalimbali hususa ni misaada ya kibinadamu kama vile vyakula kitu ambacho alimpongeza rais Jakaya kikwete kwa kuwajali.
 
Rais huyo ameondoka leo nchini akisindikizwa na Rais Kikwete  asubuhi katika uwanja wa Kilimanjaro huku ziara yake hiyo ikiwa ya mafanikio makubwa baada ya maombi yake kukubaliwa.
 
 Kwa upande wa  Rais Kikwete alisema serikali ya Tanzania itaendelea kutoka misaada mbalimbali ya kibinadamu kwa serikali hiyo ya Somalia kwakua tayari ilishaanza kutoa misaada hiyo hapo awali.
 
Aliongeza kuwa tayari serikali yake ilishatoa misaada mbalimbali ikiwemo ya vyakula ambapo jumla ya tani 500 za vyakula zilishatolewa ikijumuisha mahindi na ngano.
 
Aidha Rais Kikwete alisema mbali na misaada hiyo ya vyakula pia serikali ya Tanzania ilishatoa misaada mingine ikiwemo kuisemea Somalia katika jumuiya mbalimbali juu ya matatizo ya machafuko yanayoikumba nchi hiyo.
 
Pia alisema mbali na misaada hiyo pia Tanzania itakua tayari kwaajili ya kuisaidia Somalia kwa kutoa wataalamu wake mbalimbali kwenda nchini humo pamoja na kuwapokea wataalamu wan chi hiyo hapa nchini ili kuwafundisha namna ya kuutengeneza na kuukuza uchumi wake.
 
“sisi tulishaanza zamani kuisaidia Somalia na nimeahidi kuendelea kuisaidia kwa misaada ya kibinadamu kama vyakula matibabu pamoja na kutoa wataalamu wetu kwenda kufundisha namna ya kuujenga upya uchumi wa nchi hiyo lakini sio masuala ya kiusalama kwa kutoa majeshi yetu hapana”alisema Rais Kikwete.
 
Rais Kikwete mara baada ya kumsindikiza Rais huyo alirejea mkoani Arusha tayari kwaajili ya kuelekea mkoani Kilimanjaro leo jioni kwaajili ya shughuli ya kilele cha maadhimisho ya sherehe za mazingira hapo kesho ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia