WAKAGUZI WA HESABU ZA SEREKALI WAPIGWA MSASA

Washiriki ambao ni wakaguzi na viongozi wakiwa kwenye picha ya pamoja
 
Wakaguzi wa mahesabu ya Serikali nchini wametakiwa  kufanya kazi hiyo kwa umakini kwa kufuata madili na taratibu za kazi ya ukaguzi ikiwa ni pamoja na kutowaonea au kufanya upendeleo kwa wanaowakagua ili kusaidia kuonesha dhamani ya matumizi ya fedha za Sererikali zinazotolewa kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hayo yalibainishwa jana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Ruth Malisa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wiki 3 kwa wakaguzi wa mahesabu ya Serikali  kanda ya kaskazini kutoka mikoa ya Tanga,Kilimanjaro,Arusha na Manyara mafunzo ambayo yameandaliwa na  Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.

Alisema kuwa taarifa ya wakaguzi inategemewa kwenye shughuli mbalimbali za utafiti pamoja na wataalamu mbalimbali wa serikali katika kuonesha dhamani ya fedha za Serikali,(value for money)hivyo hali hiyo itasaidia wakaguzi kugundua na kuwa na taarifa nzuri za matumizi ya fedha za serikali katika mambo mbalimbali.

“Wakaguzi wa mahesabu wanategemewa katika kutoa maelekezo ya matumizi ya fedha za Seriakali kama jengo,au mradi wowote uliotolewa fedha na Serikali kama kilichofanyika kimeendana na fedha yenyewe,hivyo ni watu muhimu na wanapaswa kupewa mafunzo”Alisema Ruth.

Kwa upande wake Mkurugenzi msaidizi wa mafunzo kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Felister Kenulembe alisema kuwa mafunzo hayo yamelengwa kuwaongezea uwezo wakaguzi hususani ni kujifunza mifumo mipya ukaguzi.

Alisema kuwa wakaguzi wanatakiwa kuwa mbele katika kuifahamu mifumo mipya ya ukaguzi ili wasichanganywe na wanaoenda kuwakagua hali itakayosaidia kuandaa taarifa nzuri ambazo zinatonyesha matumizi mazuri ya fedha za Serikali.

“Mifumo ya ukaguzi inabadilika mara kwa mara maana tunatoa vipaumbele kwenye mafunzo ili wakaguzi waweze kuongeza ufanisi kwenye ukaguzi,ambapo leo mafunzo haya pia tumefanyia kwenye jengo letu la wakaguzi  Mkoa wa Kilimanjaro ili kupunguza garama”Alisema  Felister .

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia