Rais mstaafu Benjamini mkapa akisoma hutuba yake katika mkutano wa ICF
waandishi wa habari wakijadili jambo mara baada ya kutoka kwenye mkutano wa ICF
Mtendaji Mkuu wa ICF, Omary Issa amesema kuwa ICF imesaidia kuboresha mfumo wa usajili wa makampuni nchini
Rwanda ambapo kwa sasa humchukua mtu siku 2 kusajili biashara tofauti na awali
ambapo ilikuwa wakitumia mpaka siku 16 huku gharama zikipungua kutoka dola za
Marekani 433 mpaka 25.
Issa alisema kuwa taasisi yake katika kuhakikisha shughuli
za biashara zinafanyika kwa urahisi na ufanisi zaidi imesaidia kuboresha mfumo
wa mahakama nchini Zambia kwenye mahakama 3 na kutoa mafunzo kwa majaji wapya 14
huku nchini Sierra Leone wakifanikiwa kuboresha mfumo wa mahakama ambapo kwa
sasa huchukua miezi miwili tokea kufungua kesi za biashara na kupata uamuzi ambapo
awali ilikuwa inatumia mpaka miaka sita
alisema kuwa taasisi
hiyo inashirikiana na TRA na Jeshi la
polisi nchini kuboresha utoaji huduma kwa kuhakikisha bidhaa zinazopita nchini (transit
goods) kwenda nchi jirani ya Rwanda zinasafirishwa kwa usalama na haraka kutoka
jijini Dar es Salaam mpaka Rusumo kwenye mpaka wa nchi hizo hivyo kupunguza
gharama za usafirishaji.
Hayo yalisemwa na afisa wa TRA, Alexander Buchafwe,
alipokuwa akitoa maelezo kwenye banda ya
taasisi za serikali za nchi za Afrika zilizonufaika na Taasisi ya kuboresha
uwekezaji Afrika (ICF) ambayo inafanya mkutano wake pili mkubwa wa kimataifa kwenye hoteli ya Naura Spring.
Alisema kuwa mfumo huo ulizinduliwa rasmi Machi 12, mwaka
huu ambapo wamewapa wamiliki wote wa magari ya mizigo muda wa miezi mitatu wawe
wamefunga vifaa hivyo kutoka kwa makampuni sita waliothibitishwa na TRA kwa
ajili ya kufanya kazi ya kuuza na kufunga vifaa hivyo.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia