Ticker

6/recent/ticker-posts

ALIYEKUWA MWANACHAMA WA TATU WA CHAMA CHA NCCR MAGEUZI AMBAYE PIA NI MUHASISI WA TATU WA CHAMA HICHO AZIKWA KWA HESHIMA ZOTE

 Askofu mkuu wa KKKT kanda ya dayosisi ya kaskazini Thomas Laizer akiwa anauombea mwili wa aliyekuwa muhasisi wa chama cha NCCR mageuzi katika ibada ya kumuombea iliyofanyika katika kanisa la OLigilai
 viongozi wa NCCR mageuzi wakiwa mbele ya jeneza la marehemu Emanuel Petro Sirikwa muasisi wa chama  hicho na mwanachama mwenye kadi namba tatu
 Mwenyekiti wa chama cha NCCR mageuzi  Jemsi Mbatia akitoa salam za chama

Vijana wa chama cha NCCR mageuzi wakiwa wamebeba jeneza la muhasisi wa chama hicho wakiongozwa na mtoto wa marehemu kuelekea makaburini
 Mbunge wa viti maalum ambaye pia ni mbunge wa bunge la jumuiya ya Afrika mashariki kupitia tiketi ya chama cha NCCR mageuzi akiweka shada la maua
 Askofu akiendesha misa ya mazishi makaburini
 Alikuwa waziri mkuu ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Monduli Edward Lowasa na mke wake wakiweka shada la maua
Mke wa marehemu akiwa anaweka shada la maua katika kaburi la mume wake Emanuel Petro Sirikwa


Vyama vya siasa vimeaswa kuacha tabia ya kuchukiana na kutoleana matamko ambayo hajajengi wala kusaidia jamii nabadala yake vyama hivyo vinatakiwa kuhakikisha kuwa vinabishana kwa hoja na maelezo ambayo yanajitosheleza ili kuweza kuepusha migogoro mbalimbali ambayo inachangia sana kutokuwepo kwa amani nchini

Kauli hiyo imetolewa na Askofu Thomas Laizer wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania(KKKT)dayosisi ya  kaskazini kati wakati akiongea na waombolezaji mbalimbali katika mazishi ya aliyekuwa muhasisi wa chama cha NCCR Mageuzi Bw Emanuel Kisarika mapema jana Mjini hapa

Askofu huyo alisema kuwa kwa sasa asilimia kubwa sana ya viongozi wa vyama vya siasa wanatumia muda wao mwingi sana kupambana na kutoa matamko ambayo hayajengi taifa huku hali hiyo ikichangia kwa wingi sana kuwepo kwa mvurugiko wa amani ya nchi

Aliongeza kuwa endapo kama vyama vya siasa vingekuwa na utaratibu wa kupendana wao kwa wao basi wangechangia kwa kiwango kikubwa sana hata wananchi wa Tanzania kuwa na Umoja lakini baadhi ya vyama vimekuwa vikitumia vibaya nafasi zao za katika jamii hata kuhasisha vitu ambavyo havifai kabisa

“leo vyama vinachukiana vinatoleana maneno mabaya sana sasa haya maneno yanachangia kwa kiwango kikubwa sana kuweza kuhatarisha hata amani ya nchi ni vema kama vikiacha hivyo na hata kuangalia sasa changamoto mbalimbali ambazo zinaikabili jamii husika:”aliongeza Askofu huyo

Pia alisema kuwa kama vyama hivyo vya siasa vitakuwa na muonekano mzuri wa hoja basi vitaweza kupunguza hata matatizo mbalimbali ambayo yapo kwenye jamii hasa tatizo la ukosefu wa umoja hasa kwenye matatizo ya kijamii kama vile msiba kwa madai kuwa ni itikadi za kisiasa

‘wapo watu wanaoelewa siasa kwa mtizamo wa tofauti sana kwa  baadhi yao sasa wanaacha hata kusaidiana kutokana na itikadi za kivyama lakini kama siasa ya sasa itakuwa ni siasa ya upendo basi itachangia kwa kiwango kikubwa sana kuweza kuwarudisha hawa watu sehemu moja na kudumisha umoja ambao sasa unamezwa na uhaba wa maarifa kutokana na mfumuko wa siasa ambao upo hapa nchini kwa sasa”aliongeza Askofu Laizer

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi hapa nchini Bw James Mbatia alisema kuwa watanzania wa leo wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanakuwa nan uzalendo wa kweli kama alivyo kuwa muhasisi wa chama hicho Bw Emanuel Kasarika kwani uzalendo huo ni msingi mzuri sana wa kuweza kuimarisha hata masuala mbalimbali hapa nchini

Bw Mbatia alisema kuwa endapo kama uzalendo  wa vyama mbalimbali utaweza kudumishwa basi wataweza hata kutatua matatizo mbalimbali ambayo yapo kwenye jamii kwa uraisi sana tofauti na pale ambapo watu wanakosa uzalendo na vyama vyao pamoja na nchi yao huku hali hiyo ikichangia sana umaskini ambao umekithiri sana.

Post a Comment

0 Comments