Ticker

6/recent/ticker-posts

WATANZANIA WATAKIWA KUPIGIA KURA VIVUTIO VYA HAPA NCHINI

Shirika la hifadhi za taifa (TANAPA)wamewataka watanzania kuipigia kura vivutio vya asili barani Afrika ikiwemo Mlima Kilimanjaro,Bonde la hifadhi za Ngorongoro,na Mbuga ya Serengeti iliviweze kuingia kwenye shindano la kutafuta maajabu saba ya asili ulimwenguni.

Akizungumza na libeneke la kaskazini Meneja mahusiano wa shirika hilo Pascal Shelutete alisema kuwa Tanzania imebahatika kuingiza vivutio hivyo na kuwataka Watanzania kuipigia kura vivutio hivyo kwani Serengeti imeweza kingizwa kwa sababu ya kuhama kwa wanyama  aina ya nyumbu,kwani ni tukio adimu hapa ulimwenguni.

Alisema kuwa wapiga kura wanatakiwa kuchagua vivutio hivyo na kuvipigia kura iliviweze kupita na pia unatakiwa kuongeza vivutio vingine 4 unavyovifahamu ilikuweza kupata vivutio saba vilivyopo barani Afrika na kuuelezea mlima Kilimanjaro upo kwenye mstari wa tropiki na ni joto lakini unatheluji ambayo haikauki kwa majira yote.

Shelutete alisema kuwa utaratibu wa kupiga kura unatumika kwa kutumia barua pepe na kuwa wao kama tanapa wanashirikiana na wadau mbali mbali nkuweza kuona kuwa Tanzania inaingizwa kwenye moja ya maajabu hayo saba.

Aidha alisema kuwa mbali na kuwataka kupiga kura pia wanaendelea kuwahamasisha watanzania wakishirikiana na wadau mbali mbali ilikuweza kuwafahamisha watapata faida gani watanzania ilikuweza kuwahamasisha wale wote waliotembelea kwenye mbuga wakiwa ni wageni na watanzania kuweza kupigia kura vivutio hivyo.

Shelutete Faida tunayoipata ni kuendele kuvitangaza vivutio hivyo kwenye mataifa mbali mbali hivyo tutaweza kuongeza wageni watakaokuja kutembelea vivutio hivyo na kuongeza pato la uchumi na la taifa hadi sasa waratibu wa shindano hili hawajatoa nani yupo kwenye nafasi ipi lakini tunaimani kuwa hadi ifikapo mwezi wa December ambapo shindani hilo litafikia tamati ya upigaji kura tunaimani nasi tutakuwa ni mojawapo ya maajabu hayo ya afrika.

Shelutete alisema kuwa Shindano la kuchagua maajabu saba ya Afrika limeandaliwa na shirika la Seven Natural Wonders lenye makao yake makuu Texsas Nchini marekani na madhumuni ya shindano hili ni kutafuta maajabu saba ya Ulimwengu na kutoa sifa ya mbuga ya Serengeti ambapo kwa miezi 12 wanyama wanahama kutoka eneo moja kwenda nchi kufuta malisho.


Post a Comment

0 Comments