Ticker

6/recent/ticker-posts

KAMBI YA VIGOGO YAWATIKISA VIGOGO CCM ARUSHA

KATIKA kile kinachoonekana ni   kujiimarisha kuelekea uchaguzi mkuu wa urais mwaka 2015 kambi inayohusishwa na  waziri  mkuu mstaafu  aliyejizulu,Edward Lowasa imeibuka kidedea katika uchaguzi mkuu wa CCM wilaya ya Arusha mjini.

Katika uchaguzi huo uliokuwa na kila aina ya vituko mwenyekiti wa zamani wa CCM wilaya ya Arusha,Jubilate Kileo aliangushwa vibaya na mpinzani wake,Dk Wilfred Ole Soilel  ambaye ni daktari wa hospitali ya St,Elizabeth  kwa tofauti ya kura 70 .

Kinyanganyiro kingine kilikuwa kwenye nafasi ya mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM taifa(Nec) ambapo,Godrey Mwalusamba ambaye ni mwenyekiti wa UVCCM wilaya alifanikiwa kupata kura 449 na kuwaangusha vibaya wapinzani wake ambao ni ,Loota Laiser aliyepata kura 79 na Dk Harold Adamson aliyeambulia kura 7.

Kitendo cha wajumbe wa mkutano mkuu kumchagua Dk Ole Soilel anayehusishwa na kambi la Lowasa kuliibua simanzi kwa kambi nyingine ambapo katika hali isiyo ya kawaida mkuu wa mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo sanjari na katibu wa CCM Arusha,Mary Chatanda juzi walionekana kuwa wanyonge muda wote kitendo kilichoibua maswali mengi  kwa baadhi ya wajumbe waliohudhuria uchaguzi huo.

Katika hali isiyo ya kawaida Kileo pamoja na wafuasi wake walikacha kabla ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi huo lakini alipotafutwa na gazeti hili kwa njia ya simu alikataa kuweka wazi endapo ameridhika na matokeo ya uchaguzi huo na kudai kwamba kilichofanyika ni kuondoa kundi moja na kuingiza kundi lingine.

 Hatahivyo,kijana mmoja ambaye ametajwa kuwa ni mfuasi wa kundi la Kileo alipewa kichapo nje ya ukumbi wa uchaguzi ndani ya hoteli ya Naura jijini hapa kwa kile kinachodaiwa ni kutoa lugha chafu kwa  wafuasi wa Musa Mkanga ambaye naye alikuwa akiwania nafasi ya uenyekiti wa CCM wilaya.

Awali kabla ya uchaguzi huo taarifa zilizolifikia LIBENEKE LA KASKAZINI  zimedai ya kwamba ndani ya ukumbi wa uchaguzi Kileo aliulizwa maswali na wajumbe wa mkutano huo kwamba aeleze sababu za yeye kushindwa kusimamia jimbo la Arusha mjini lililoangukia upinzani pamoja na kata yake ya Kaloleni hali iliyompa wakati mgumu kujibu maswali hayo.

Hatahivyo,taarifa zilizowakariri baadhi ya wajumbe ndani ya mkutano huo zimedai kwamba Kileo nusura aangue kilio ambapo alikaririwa akiwaambia wajumbe ya kwamba wamhurumie kwa kuwa yeye ni mzee na endapo akichukia itakuwa laana kwao.

“Kileo alipigwa swali kwamba yeye kama mwenyekiti wa wilaya kwanini hakusimamia jimbo hadi likaangukia upinzani lakini pamoja na kata yake ya Kaloleni ndipo akajibu kwamba yeye ni mzee wamhurumie kwani akichukia huenda akawaachia laana”kilisema chanzo cha habari ndani ya mkutano huo

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo,katibu wa CCM wilaya ya Longido,Esupat Naikaya alitangaza nafasi ya uenyekiti wa wilaya na kusema kwamba kura halali zilizopigwa ni 538 ambapo wagombea Musa Mkanga alipata kura 1,Jubilate Kileo alipata kura 232 na Dk,Wilfred Ole Soilel alipata kura 305 na kutangazwa mshindi.

Wengine waliotangazwa ni wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM kuwa ni mkuu wa mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo,Halima Mamuya,Fatuma Ngairo,Musa Mkanga pamoja na Getrude Haule.

Kwa upande wa wajumbe wawakilishi wa mkutano mkuu wa CCM mkoa waliotangazwa washindi ni Agrey Mushi pamoja na Gasper Kishumbua .

Awali  akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi mwenyekiti mteule wa CCM wilaya,Dk Ole Soilel aliwashukuru wajumbe waliompatia kura na kuwaambia kwamba wana kibarua kikubwa cha kuhakikisha wanapambana na upinzani uliojiimarisha wilayani Arusha.

“Tuna kibarua kikubwa cha kupambana na upinzani hapa Arusha nyine ni mashahidi hapa mjini bendera za wapinzani zimeenea kila kona za kwetu hakuna kama kwamba CCM sio chama tawala”alisema Ole Soilel

Naye,Mwalusamba pamoja na mkuu wa mkoa wa Arusha,Mulongo waliwashukuru wajumbe waliowapatia kura katika uchaguzi huo huku wakihaidi kuwatumikia katika uongozi uliotukuka.

kwa upande wa wilaya ya simanjiro Mbunge wa jimbo la Simanjiro Christopher ole sendeka ameweza kupeta mara baada yakumshinda mpinzani wake Justine Nyari kwa kura345 ambapo wapinzani wengine ambao ni lenganasa pamoja na Awazo Omary walijito.

Katika kura hizo jumla ya wapiga kura 610 walishiriki na sendeka aliweza kupata kura 471 huku nyari akipata kura 126 kwa upande wa wenyekiti wa wilaya Broun Methius ole suye aliweza kupata kura 423 na kunyakuwa nafasi hiyo huku lengai Ole Makooo akipata kura 198.

mara baada ya sendeka kutangazwa mshindi aliwashukuru wananchi wa wilaya hiyo nakubainisha kuwa ata endelea kuwasaidia wananchi wa wilaya hiyo kwa hali namali.

kwa upande wa wilaya ya Babati vijijini  nafasi ya mwenyekiti imechukuliwa na Alhaji Songora ambaye amepata kura 656 ambapo mpinzani wake Laurenti Fisso akipataa kura 264 na upande wa NEC Amani Hilji alipeta kwakupata kura 531 na mpinzani wake Willy Bayo akipata kura 362  huku nafasi wa tatu Peter Naali akipata kura 84 .

Post a Comment

0 Comments