WATU MILIONI TATU WANUFAIKA NA MIRADI KUTOKA KITUO CHA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

Kituo cha  Mafunzo ya Ujasiriamali Tanzania chenye  makao yake makuu mjini Daresalaam kiatarajia kunufaisha watu kati ya milioni  mbili na milioni  tatu katika wilaya 56 za Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar


Mkurugenzi  wa Kituo hicho hapa nchini  Mbutolwe Lucy Mwaipopo amesema hayo  mjini  Kahama  jana alipokuwa akieleleza  mikakati ya kituo hicho


 Mwaipopo alisema  lengo la kituo ni kuwafikia kaya zaidi ya  20,000 maskini zene watu kati 100,000 na  laki  300,000 ifikapo mwaka 2015


 Alisema  watu hao wapatiwa ngombe  na  mbuzi wa kisasa  na  kuku  pamoja na kujengewa mabwawa ya samaki kwa njia ya ruzuku awamu hii ya kwanza


Mkurugenzi  Mwaipopo  amesisitiza kuwa program hii niya miaka kumi na inatakelezwa na taasisi hiyo  kama sekta binafsi na Serikali (PPP) kwa ufadhili wa Shirika  la Misaada la Uingereza DFID


 Mwaipopo amefafanua kuwa  mradi huu unawalenga  zaidi kaya maskini  hususani   wanawake wajane, wasio na uwezo kiuchumi


Aidha amefaanua  kuwa mradi unawalenda pia watu wengine wa kipato cha chini  na wenye utashi wa ufugaji na ambao wataweza kuendeleza miradi hii kwa hiari yao ili kuinua kipato chao


 Mwaipopo amesema mradi huo  hivi sasa unatekelezwa  katika Mikoa ya Shinyanga,Morogoro, Iringa,Dodoma, Mbeya, Tabora na Zanzibar na Pemba katika  awamu ya kwanza ifikapo mwaka 2015


Mkurugenzi  Mwaipopo aidha amesema mradi huu unatarajia kutekelezwa   katika   mikoa ya Kagera,Mara,Kigoma ifikapo mwaka 2025 ili kufikia malengo ya Mellenia


Naye Daktari wa mifugo katika taasisi hiyo Dakta Herman Kamwela amesema ili  mtu aweze kunufaika na mradi huo lazima kwanza ahudhurie mafunzo ya siku kumi


Hatua itamsaidia kumjengea uwezo  wa kutambua  mradi wenyewe na jinsi atakavyowezaa kuhudumia ambapo atafundishwa  masuala    yanayohusu afya, tiba,dalili  za magonjwa aina ya mifugo bora


Dakta Kamweleza amesisitiza kuwa  mradi huu umelenga wakomboa wananchi wa kipato ca chini kuondokana na umaskini unaowakabili   maelfu ya wanawake wa Tanzania hivi sasa hususani wa maeneo ya vijijini


Aidha Dakta Kamwela amesisitiza  kwamba  mradi huu utasaidia kupinguza migogoro ya chakula katika kaya vijijini  pamoja na utapiamlo katika jamii

Migogoro ya chakula bora vijijini , utapiamlo ni changamoto kubwa inayokabili familia nyingi vijijini hususani watoto wenye umri wa miaka  chini ya mitano na mama wajawazito.Alieleza Dakta Kamwela

Pia alisema chini ya mradi huu  wanufaika wa mradi huu pia hufundishwa teknolojia sasa kisasa  za ufugaji na namna ya kuhudumia mifugo kiutalaam zaidi


Hata hivyo Dakta Kamwela ametaja  baadhi ya changamoo zilizopo  ni tatizo ya upatikanaji wa madawa ya mifugo  hasa maeneo ya vijijini  na ubora wa madawa hayo


Mtalaam huyo wa sekta ya mifugo na kilimo  alisema dawa nyingi zinazongizwa nchini hussani zinazowafikia wafugaji vijijini ni zile ambazo muda wake umekwsha  na mbazo hazifai kwa matumizi


Ametaja baadhi ya mikakati ya taasisi hiyo kuwa ni kujenga majosho ya kisasa  yasiyotumia maji mengi katika kila kijiji cha mradi

aidha taasisi hiyo amesema taasisi pia inatarajia kuanzisha madawa   ya mifugo katika kila wilaya ili kupunguza  kero kwa wafugaji

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia