GOROMAIYA KUKIPIGA NA SIMBA


mmoja wa wachezaji wa simba akiwa ameumia katika mazoezi 
kocha wa simba akiwa anawapa mazoezi wachezaji wake katika uwanja wa shule ya st.Jude jijini Arusha
Timu ya simba ambayo imeweka kambi jijini hapa kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya ligi ya vodacom Agosti 18  mwaka huu inatarajia kucheza mechi yakirafiki na timu ya Goromaiya ya  nchini kenya katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheirkh Amri Abeid jijini hapa.
Akiongea na waandishi wa habari  mwenyekiti wa klabu ya simba jijjini hapa Afrey Mkumbo alisema kuwa  mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa juma mosi majira saa kumi katika uwanja  huo.
Alisema mechi hii ya kirafiki itakuwa ni moja ya mechi ambazo wameziweka katika ratiba zao ambapo alisema kuwa mbali na mechi hiyo pia wanampango wa kucheza  na timu ya chaki ya jijini hapa.
Aidha alisema kuwa walikuwa na mpango wa kucheza mechi ya kirafiki na timu ya jkt oljoro lakini wameshindwa kutokana na timu hiyo kutokuwa na wachezaji wote hali ambayo ilisabisha kocha wa tim u ya simba kugoma kupeleka wachezaji mbulu katika mechi hiyo ambapo alidai kuwa ni bora wakapoteza mechi hiyo ya kirafiki.
Kwa upande wake kocha wa timu ya simba Mserbia Profesa Milovan Cirkovick alisema kuwa mpaka sasa mazoezi yanaenda vyema na hakuna mchezai hata mmoja ambaye ni majeruhi na aliisifia hali ya hewa na kusema kuwa kwa sasa hali ya hewa ni mzuri na inawazezesha wachezaji kufanya mazoezi pasipo kuchoka.

Alibainisha kuwa  katika siku ya kwanza ya mazoezi yao na kikosi hicho  wachezaji wote wameonyesha viwango vya hali ya juu aku akimsifia mchezaji mshambuliaji Akuffo ni hatari mno na kwa haraka haraka hakuna wa kumfananisha naye kati ya washambuliaji wote waliopo Tanzania kwa sasa.


Alisema  kuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira, kasi, nguvu, ufundi na mbinu za kimchezo maana yake Wekundu wa Msimbazi wamepata kiongo mwenye vigezo.


Wachezaji wengine wa kigeni kwenye kikosi cha Simba SC ni washambuliaji Mganda Emmanuel Okwi na Mzambia Felix Sunzu ambapo kwa upande wa mchezaji okwi yeye anatarajiwa kuwasili kambini kesho

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post