WAENDESHA PIKIPIKI WAGOMA KULIPA USHURU


Waendesha pikipiki  alimaarufu boda boda mkoani Arusha leo wamegoma kwa muda usiopungua masaa sita wakipinga ongezeko la tozo ya halmashauri kulipa shilingi 500 kwa ajili ya ushuru wa magesho .

Wakizungumza kwa jaziba na kaimu kamanda wa polisi mkoa arusha wambura walisema kuwa wamepat atangazo linalowataka kulipa ushuru wa shilingi 500 kwa maegesho kwa kwasiku hali ambayo wamesema hawakubaliani nayo kutokana na kutokuwa na fedha za kulipa ushuru huo ambapo walisema kuwa watakuwa wanaumizwa.

Akiongea kwa niaba ya wenzake mwenyekiti wa chama cha waendesha pikipiki mkoa wa Arusha Godlight Rungamulila alisema kuwa fedha hiyo la maegesho ni kubwa sana kwa wao waendesha pikipiki kwani ukipiga esabu kwa mwaka mzima inakuwa nyingi sana na ukichanganya na ushuru ambao wanalipa pamoja na Trl wanakuwa wanawaumiza sana waendesha pikipiki na pia alibainisha kuwa kinachowaumiza ni kwamba bei hiyo imepandishwa pasipo kushirikishwa wakati wao ndi wahusika .

“unajua serekali ilitutolea bei ya maegesho kwa waendesha pikipiki ambapo tulikuwa tunalipa shilingi 35000kwa mwaka sasa wanavyo tuambia tulipe shilingi 500 kwa siku si wanatukomoa kwani  fedha hizo ni nyingi sana na hata  ukipiga hesabu inakuja mara nne ya ile serekali ambayo imetufutia sasa sibora wangeacha ile kuliko  kutuambia tulipe hela hii kwa siku”alisema mwenyekiti

Aidha mgogoro huo uliendelea hadi pale mkuu wa wilaya ya arusha  John Mongela alipokuja na kutatua swala hilo ambapo aliwataka  warudi katika sehemu zao za kazi na kusema kuwa wao wenyewe kama serekali hawajui swala hili na wala mkurugenzi hajui hivyo  tangazo hilo ni batili.

Alisema kuwa wao kama serekali ya mkoa na wilaya wameanza kulishulikia swala hili na hadi kufikia sasa wameshamjua aliyetoa tangazo hilo na wapo katika harakati za kumchukulia hatua kali na kuwahaidi waendesha pikipiki hao kuwa ndani ya siku mbili watakuwa wameshachukuliwa hatua za kisheria..

“kiukweli mimi nilikuwa sikjui wala mkuu wa mkoa na mkurugenzi  na hatuwezi kupandisha  bei ya maegesho pasipo kuwashirikisha nyie sisi tutawashirikisha na tutahakikisha tunakuliana ndo tufanye hivi la kini hatuwezi kukurupuka na kujichukulia sheria mkononi sisi tunafanya kazi kwa kufuata utaratibu na kanuni  lakini napenda kuwaambia kuwa swala hili lililkuwepo katika mazungumzo na muafaka bado na kwanza bado sana hivyo mtu huyu aliotoa tangazo hili ni muongo sio mkweli na tangazo hili ni batili rudini vijiweni kwenu mkafanye kazi mtu yeyote asiwachaji ushuru’alisema Mongela.

Aliwataka kufuata sheria za barabarani ili kupunguza ajali ambazo zinatokea mara kwa mara  na pia aliwasihi kutofanya fujo ambazo zisizokuwa na mahana bali kufikiria kabla ya kufanya jambo.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post