Ticker

6/recent/ticker-posts

WAISLAM ARUSHA WAPINGA UTEUZI WA MAKADHI


UAMUZI wa kupinga uteuzi wa kadhi mkuu na makadhi wa mikoa 14 uliofanywa na Sheikh Mkuu wa Tanzania,Mufti Shaaban Simba umezidi kupingwa vikali  baada ya baadhi ya viongozi na waumini wa dini hiyo mkoani hapa kuupinga kwa nguvu zote huku  wakisema ya kwamba uteuzi huo unalenga kuwavuruga waislamu nchini.

Hivi karibuni Mufti Simba alimtangaza  Sheikh Abdallah Mnyasi kuwa kadhi mkuu na pia aliwateua manaibu wake wawili,Sheikh Abubakar Zubeir na Sheikh Muhidini Mkoyogole.

Akipinga uteuzi huo,Imamu wa msikiti mkuu mkoani Arusha,Mohammed Hambal alisema kwamba uteuzi huo una makosa makubwa kwa kuwa kadhi mkuu huteuliwa na jopo la wasomi na sio mtu mmoja.

Alihoji  kwamba taifa liko kwenye hatua ya uundwaji wa mchakato wa katiba mpya kwa sasa na kilio cha waislamu nchini ni uundwaji wa mahakama ya kadhi iingizwe kwenye katiba hiyo na kushangaa uteuzi huo kufanyika wakati huu.

“Wakati tume ya kukusanya maoni ikipita tunashangaa Mufti anamteua Kadhi mkuu kitu ambacho ni kinyume na taratibu na mwogozo wa nchi”alisema Hambal

Hatahivyo,Hambal alihoji uteuzi huo umezingatia katiba ipi kwa kuwa katiba ya nchi pamoja na katiba ya Bakwata haina kpengere wala maelekezo ya mfumo wa uundwaji wa Mahakama ya kadhi.

Naye,mwenyekti wa msikiti huo.Abdulazizi Mkindi alisema kwamba amepokea uteuzi wa Mufti kwa masikitiko makubwa kwa kuwa uteuzi huo umefanywa na kikundi cha watu wachache kwa lengo la kuwaongoza wailsamu nchini na taasisi zao.

Alisema kwamba masuala ya uteuzi wa Kadhi mkuu  yanapaswa kusimamiwa na watalaamu na wasomi waliobobea katika sheria na sharia za kiislamu na si vinginevyo.

“Kilio cha mahakama ya kadhi ni kilio cha wailsamu wote na si kilio cha Bakwata pekee,masuala ya kadhi yanatakiwa yasimamiwe na wataalamu waliosomea sheria na sharia za kiislamu na si watu wa hovyo”alisema Mkindi

Mustapha Kihago sanjari na Salim Mvungi  maarufu kama Shefu kwa upande wao walipinga uteuzi huo na kusema kwamba wameshutushwa na wanahisi kwamba hizo ni  njama za serikali kuitumia taasisi ya Bakwata kuwavuruga wasilamu nchini.

Walimnyooshea vidole  Mufti Simba kuwa amelifanya suala la uteuzi wa Kadhi mkuu kama ajenda yake binafsi wakati jambo hilo ni la wailsamu wote nchini.

Post a Comment

0 Comments