Ticker

6/recent/ticker-posts

VIONGOZI WA TASO WATAKIWA KUTOA TADHIMINI KWA WAKULIMA


Viongozi wa chama cha wakulima na wafugaji kanda ya kaskazini (TASO)  wametakiwa kuta tathimini ya wakulima na wafugaji wangapi ambao wamefaidi maonysho hayo tangu kuanza kwake.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa manyara Erasto Bwilo wakati w a ufunguzi rasmi maonysho ya wakulima na wafugaji  yanane nane yanayofanyika katika viwanja vya Taso themi  njiro jijini hapa

“wanacchi wamekuwa wakijiliza juu ya faida znazopatikana kutokana na maonyesho hayo bila kupata jibu na kubaki ikinung’funika wasijue cha kufanya “alisema mkuu huyo

Akifafanua zaidi alisema kuwa taso wanapaswa kujiwekea mikakati katika shughuli zote wanazofanya ili kuondoa kuauli ya sitofahamu na kuwashindanisha wakulima hao na kuwapa zawadi.

 Aidha alisema kuwa taso inapaswa kuhakikisha inapeleka teknolojia ya kilimo na pembejeio na ufugaji  vijijini ili kuweza kuleta ushindani katika maonyesho mengine

Naye mwenyekiti wa taso kanda ya kaskazini Arthur Kitonga alimtaka mkuu hyo wa mkoa  kuhakikisha anashirikiana nao ili kuweza kujenga hosteli

Hata hivyo alimkumbusha waziri aliyekuwa na dhamana wa kilimo Profesa Jumanne Maghembe kutekeleza ahadi ya shilingi milioni 300 ya kungania kujengwa kwa hostel ndani ya uwanja huo wa maonyesho aliyoitoa mwaka jana kwa ajili ya wakulima

 Maonyesho hayo ya wakulima na wafugaji ni ya 9 tangu kuanzishwa kwake na uadhimishwa kila mwaka na kuwakutanisha wakulima na wafugaji pamoja na wadau mbalimbali na kwa mwaka huu yanatarajiwa kufugwa na waziri mkuu muheshimiwa mizengo pinda

Post a Comment

0 Comments