MALULA SEKONDARI WALIA NA KERO YA MAJI

UONGOZI wa shule ya sekondari ya Malula iliyopo King”ori wilayani Arumeru Mashariki mkoani Arusha umeiangukia serikali na kuiomba itatue tatizo la kero ya maji inayowakabili shuleni hapo kwa madai kwamba linachangia kudumaza kiwango cha elimu shuleni hapo.

Hatahivyo,uongozi huo umesisitiza ya kwamba wanafunzi wa shule hiyo wanalazimika kutembea umbali mrefu kusaka huduma hiyo na kujikuta wakipoteza muda mwingi wa masomo.

Akizungumza katika mahafali ya kwanza shuleni hapo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mkuu wa shule hiyo,Rehema Mroso alisema kwamba shule yake imekuwa ikikabiliwa na tatizo kuu la uhaba wa maji tangu ianzishwe huku akiiomba serikali iwajengee matanki ya kuhifadhi maji kuokoa tatizo hilo.

Mroso,alisema kwamba baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wanalazimika kutembea umbali mrefu wa zaidi ya kolomita 5 kusaka maji kitendo ambacho kimechangia kudumaza kiwango chao cha elimu kwa kuwa wanatumia muda mwingi kusaka maji.

Alisema kwamba tatizo la uhabaw a maji limechangia kuharibu mazingira shuleni hapo kwa kuwa hukosa maji ya kuboreshea mazingira sanjari na kusafishia vyoo mbalimbali shuleni hapo.

“Tuna tatizo kubwa la maji hapa shuleni kwetu wanafunzi hutembea hadi Kia kusaka maji na kujikutab wanatumia muda mwingi kuyasaka maji na kisha kupoteza muda wa masomo’alisema Mroso

Hatahivyo,alisisitiza kwamba wamekuwa wakibaliwa na kero za uhaba wa jengo la utawala,maabara,uhaba wa nyumba za walimu sanjari na tatizo la uzio wa shule hali ambayo inahatarisha usalama wa wanafunzi hususani wa kike wanaolala shuleni hapo.

Awali akizungumza katika mahafali hayo mgeni ramsi ambaye alikuwan ni katubu tawala wa mkoa wa Arusha,Exauds Mwanga alisema kwamba serikali imepokea  na italifanyia kazi  tatizo la kero ya maji lakini aliwashauri kupanda miti ya kutosha kwa lengo la kuhifadhi  mazingira shuleni hapo.

Mwanga,alikemea tabia ya baadhi ya wanfunzi hususani wa kiume shuleni hapo kuvaa suruali zao chini ya makalio maarufu kama  “mlegezo” huku akisisitiza ya kwamba uvaaji huo ni marufuku hapa nchini.

Hatahivyo,alisisitiza kwa ukali kwamba serikali itawachukulia hatua kali wale watakaobainika kununua mitihani ya kidato cha nne na kudai kwamba wazazi wa wanafunzi watakaowasaidia watoto wao kununua mtihani hiyo nao watakiona cha moto.

“Nimesema kwamba endapo mwaka huu Yule atakayebainika kununua mtihani iwe mwalimu,mwanafunzi ama mzazi nitakufa naye narudia tena nitakufa naye”alisema Mwanga

Aliwataka wazazi wa wanafunzi hao kuwaandaa watoto wao kwa ajili ya mitihani ya kidato cha  nne na sio kuwapatia fedha za kununulia mitihani hiyo.


About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia