Ticker

6/recent/ticker-posts

WANANCHI KIDEGEMBYE WAFUNGA OFISI ZA KATA NA KIJIJI

Wananchi wa kijiji cha kata ya Kidegembye  Wilayani Njombe wamewakataa viongozi wa kata na kijiji hicho huku ofisi za viongozi hao za kijiji na kata zikifungwa  kwa muda wa siku saba hadi leo bila kufanya kazi na kufunguliwa kwake hadi watakapo maliziwa matatizo wanayokabiliwa.

Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo mbele ya afisa taaraafa aliyekwenda kusikiliza matatizo yao kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Njombe  Sarah Dumba wamesema sababu za kufunga ofisi hizo ni kutokana na hujuma za mali za kijiji zilizofanyika na uongozi wa kijiji na kata hiyo ikiwemo kutowa somea hesabu za mapato na matumizi ya michango ya shule ya sekondari Kidegembye kwa muda wa miaka mine sasa.

Aidha wananchi hao wamesema mbali na hayo sababu nyingine iliyowafanya waukatae uongozi wao wa kata na kijiji kuwa ni pamoja na diwani wao kuhujumu michango ya wananchi ya ujenzi wa madarasa na kuendeleza majengo ya shule ya sekondari  kidegembye akiwa mwenyekiti wa bodi ya shule.

Halikadharika madai mengine ya wananchi hao ni kwamba diwani wa kata hiyo amekuwa akitumia madaraka vibaya kwa kuwanyang’anya mali zao zilizopo mpakani mwa shule ya sekondari kidegembye kwa kupitia mgongo wa shule hiyo kwa maslahi binafsi,kutumia mfumo wa kidikiteta katika utawala wake,ahadi za uongo, ,huku mtendaji wa kijiji akiwa mlevi kupindukia hali iliyomfanya apoteze kitabu cha ushuru,kuhusika na wizi wa mawe na kuwalea na kuwalinda vijana wezi  .

Pamoja na hayo wananchi hao wamesema kwa upande wa mwenyekiti wa kijiji hicho wanamutuhumu kwa kosa la kushindwa kusimamia na kutetea haki na mali za wananchi pindi wanapovamiwa katika maeneo yao,kushindwa kutambua kuwatawala  kimaadili,kanuni na sheria za uongozi kwani amekuwa akitawaliwa na diwani pamoja na mtendaji wa kijiji hicho.

Sanjali na hayo wananchi hao wamesema kuwa kutokana na matatizo walioyaodhesha hapo juu ilipelekea kufunga ofisi hizo huku wakibainisha baadhi ya viongozi wa wa kata na vijiji kuwa hawastahili kuendelea kutawala kijiji hicho akiwemo diwani na mwenyekiti wa bodi  wa shule ya sekondari kidegembye,mwenyekiti wa kamati ya ujenzi na baraza la kata yote huku katika ngazi ya kijiji akiwemo mtendaji wa kijiji hicho na wajumbe wake.

Kwa mujibu wa taari yao wananchi hao mbele ya afisa taarafa iliyosomwa na Batwel Ngewe kwa niaba ya wananchi wote hawatakuwa tayari kufungua ofisi hizo endapo viongozi hao wataendelea kuwepo madarakani huku wakisema wanapoondoka madarakani wakabidhi mali zao walizopolwa.

Afisa taraafa wa Lupembe bwana Baltazary Mveyange amekili kupokea malalamiko hayo na kuahidi kuyafikisha kwa mkuu wa wilaya ya Njombe Sarah Dumba  ili kulifanyia ufumbuzi tatizo la wananchi hao huku akisema taarifa zinazowafikia viongozi wa ngazi za juu ni  tofauti na malalamiko yanayotolewa na wananchi hao.

Aidha Afisa tarafa huyo Mveyange amesema taarifa zilizotolewa na viongozi wa kata na kijiji hicho cha kidegembye ni kwamba wanaolalamikia kunyang’anywa na kudhurumiwa haki zao ni kikundi cha watu pekee lakini amekili kuwepo kwa mapungufu ya viongozi wa kata na kijiji hicho huku diwani wa kata hiyo akishindwa kuhudhuria mkutano huo na  simu yake haipatikani licha yakupewa taarifa mapema.


Mkutano huo umeahirishwa hadi wiki ijayo mara uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe akiwemo mkuu wa wilaya ya Njombe na mkuu wa shule ya sekondari kidegembye ambapo watakwenda kushuhudia maeneo yanayolalamikiwa na kusema wakati wowote katikati ya wiki watapewa taarifa juu ya ujio wa wawageni hao.

Hadi sasa viongozi wa kata na kijiji cha kidegembye mkoani Njombe wanatimiza siku ya saba bila kutumia ofisi za kijiji na kata kutokana na wananchi hao kufunga ofisi hizo huku wakipeana zamu ya kulinda wakati wa usiku na mchana ili ofisi hizo zisipatwa na tatizo la  kuvunjwa mpaka ufumbuzi utakapo patikana.


Post a Comment

1 Comments

  1. Hongera kwa kazi mnayo ifanya kwa kutuwakilisha watu wa kidegembye kwa habari motomoto.

    ReplyDelete

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia