ADHABU YA WIZI KWA MWALIMU NI KUAMISHWA ENEO LA KAZI?
Halmashauri ya wilaya ya Karatu iliyoko mkoani Arusha
imeamua kumbadilishia mazingira ya kazi mwalimu wa shule msingi ya Barakta
kupisha uchunguzi wa tuhuma za kuiba mali ya shule zinazomkabili.
Halmashauri ya wilaya ya Karatu imefikia hatua hiyo baada ya
wazazi wa wananfunzi kugoma watoto wao kuhudhuria shule kwa muda wa siku tatu
mfululizo kushinikiza kumkataa mwalimu huyo aliyejulika kama Anjelina Sarwat kutokana
na tabia hiyo ya kuiba mara kwa mara mali ya shule ikiwemo chakula
kilichotolewa msaada na mpango wa chakula duniani (WFP).
Wakiongea kwenye mkutano mkuu wa kata, ikiwa ni siku ya tatu
ya mgomo wao wananchi hao walisema kuwa wamechoshwa na tabia ya mwalimu huyo ya
kuiba mara kwa mara mali
ya shule kwa kujinufaisha yeye na familia yake ambapo pia wamemtuhumu vikali
mwalimu huyo kujihusisha na maswala ya kishirikina.
Aidha kikao hicho pia kimetokana na vilio na majonzi ya hofu
iliyotanda usiku wa septemba 28 baada ya kumkamata mtoto wa mwalimu huyo
(Paskali Raphael) katika vyanzo vya maji (mto na kisima) akinyunyizia dawa kwenye maji iliyoshirikishwa na imani za
kishirikana hali iliyoamsha hisia za watu hao na kuamua kupiga yowe usiku huo.
Hata hivyo baada ya kilio hicho viongozi wa serikali
walifika eneo la tukio na kukuta dawa hizo zilizowekwa pembezoni mwa kisima cha
maji ambayo ni tegemezi pekee kijijini hapo na kuamua kuwatuliza wananchi na
kumkamata kijana huyo kwa mahojiano ya awali ambapo alisema kuwa alichukua dawa
hizo kwa ajili ya kuwatuliza wananchi na uhasama waliyonayo dhidi ya familia
yao.
Akiongea na waandishi wa habari diwani wa kata ya Kansay
John Pissa alisema kuwa chanzo cha wazazi hao kugomea watoto wao wasiudhurie
shule ni baada ya kuchoshwa na tabia ya mwalimu huyo ya kukamatwa kwa nyakati
tofauti na mali za shule na pindi akiulizwa hudai kurejesha ikiwemo gunia la
mahindi, gunia la maharage pia ndoo ya mafuta pamoja na mabati matano ya shule
hiyo ya Barakta.
Hata hivyo baada ya mgomo huo Halmashauri ya wilaya ya
Karatu imeamua kumuamisha mwalimu huyo kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo na
kumpeleka katika shule ya msingi Ayalaliyo iliyoko wilwyw hiyo hiyo ya Karatu.
Afisa elimu shule za msingi Kinyemi Sepetu alisema
kuwa ingawa mwalimu huyo alikiri kukutwa na mabati hayo lakini alikana kuwa ni mali
ya shule na kuomba halmashauri imlinde ndipo kuamua kumuhamishia shule ya
Ayalaliyo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma hizo.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia