WAZAZI WATAKIWA KUWAJALI WATOTO WAO
Diwani wa Kata ya Endiamtu Mji mdogo
wa Mirerani Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Lucas Zacharia akimkabidhi cheti
cha kuhitimu kidato cha nne mwanafunzi wa shule ya sekondari Naisinyai,Roda
Yonah kwenye mahafali ya nne ya shule hiyo
JAMII Wilayani Simanjiro Mkoani
Manyara imetakiwa kuwajali watoto wao kwa kujenga mabweni kwani baadhi ya
wanafunzi wa shule ya sekondari Naisinyai kila siku hutembea kilomita 20 kwenda
shule na kurudi nyumbani.
Hayo yalisemwa na Diwani wa Kata
ya Endiamtu Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Lucas Zacharia kwenye
mahafali ya nne ya shule ya sekondari Naisinyai iliyopo kata ya Naisinyai wilayani humo.
Zacharia alisema kutokana na hali
hiyo baadhi ya wanafunzi wanosoma kutwa kwenye shule hiyo hulazimika kutembea kila
siku umbali wa kilomita 20 kwenda shule na kurudi nyumbani hivyo kuchangia
kushusha kiwango cha taaluma.
Alitoa wito kwa jamii inayozunguka
eneo hilo kuchangia gharama za ujenzi wa bweni la kulala wanafunzi hao kuliko
kuiachia Serikali peke yake kwani wanaoteseka ni watoto wanaozunguka eneo hilo.
“Kama mlivyosema hiyo ni changamoto
kwa jamii yetu kuchanga ili Serikali nayo itie mkono wake lakini hivi sasa
mtakuwa mnawapa walimu kazi mbili ya kufundisha na kutoa pole watoto wanapochoka
kutembea,” alisema Zacharia.
Pia,Diwani huyo alijitolea sh1
milioni na kuungana na Mwenyekiti wa kijiji cha Naisinyai Taiko Kurian
aliyechangia sh1 milioni kwa ajili ya ununuzi wa mashine ya kuweka umeme wa jua
(sola) kwani shule hiyo haina nishati ya umeme.
Akisoma risala kwenye mahafali
hayo,Mkuu wa shule hiyo,Emmanuel Kirenga alisema shule ya sekondari Naisinyai
ilianzishwa Februari 13 mwaka 2006 ikiwa na wanafunzi 101 na walimu watatu.
Mwalimu Kirenga alisema kuwa hivi
sasa shule hiyo ya sekondari Naisinyai ina wanafunzi 491 wakiwemo wahitimu 103
waliomaliza kidato cha nne na wana walimu 16 na wafanyakazi wa shule sita.
Alisema wanakabiliwa na changamoto ya
ukosefu wa mabweni ya kulala wanafunzi,utoro uliokithiri,uzio unaosababisha
mifugo kuingia shuleni na kuharibu mazingira na ukosefu wa nishati ya umeme.
Alimshukuru Zacharia kwa kuchangia
sh1 milioni ya kununua umeme wa sola na pia alitoa shukrani kwa Elibariki
Solomoni mmoja wa wazazi walio na wanafunzi shuleni hapo aliyejitolea jenereta
kwa ajili ya nishati ya umeme shuleni hapo.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia