JUMLA YA SHILINGI MIL.48ZIMEPATIKANA KATIKA HARAMBEE YA SHULE YA SEKONDARI PEACE HOUSE
Jumla ya
shilingi milioni 48 zimepatikana katika harambee ya kuchangia shule ya watoto
yatima ya Peace House iliyopo Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha
inayomilikiwa na kanisa la kiinjikli la kilutheri Tanzania.
Akizungumza
wakati wa harambee hiyo iliyoambatana na mahafali ya pili ya kidato cha nne
mgeni rasmi Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya
Kati Dkt. Thomas Laizer amesema kuwa watoto yatima ni sehemu ya jamii
hivyo ni vyema kama jamii itabadili mtizamo yao na kuwapatia haki sawa
iliwaweze kufikia malengo yao kama ilivyo kwa watoto wengine.
Dkt.Laizer
amesema kuwa jamii imekuwa ikiwatenga watoto yatima haswa ndugu wa yatima hao
hali ambayo inapelekea kukosa mahitaji ya msingi kama elimu.
Aidha
amesema kuwa watoto yatima wanahitaji mahitaji
muhimu kama walivyo watoto wengine na pindi wanapopata nafasi ya
kujiendeleza kielimu daima huwa wananfanya vizuri.
Pia
amewahimiza watanzania kuendelea kuwasaidia yatima bila kusubiri wafadhili
kutoka nje kwa kuwa vitabu vitakatifu vya dini vinahimiza kuwasaidia watoto
hawa ambao wengi wao wamejaa sononeko la kuondokewa na wazazi wao.
Kwa upande
wake mkuu wa shule hiyo Christopher Augustine Mushi amemshukuru baba Askofu na
wadau wote waliochangia harambee hiyo kwa kuwa wamesaidia kwa kiasi kikubwa
kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili kwa sasa ambapo itakumbukwa kuwa
wafadhili wa shule hiyo walijitioa kufadhili.
Mushi
amesema kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi kutokana na hapo awali
ilikuwa inafadhili asilimia mia moja kwa miaka mine mfululizo na ilikuwa ikichukua watoto yatima na wale
wanaoishi katika mazingira hatarishi.
Lakini mwaka
2011 taswira ya wafadhili ilibadilika gafla ambapo walitaka kufunga shule hiyo
kwa miezi 18 tangu September hadi march
2013 hali ambayo ilitoa tasiri mbaya na isiyokubalika katika sera ya elimu
sheria za nchi na jambo hili lilipigwa na bodi vikali pamoja na dayosisi katika vikao vyao mbali
vilivyofanyika .
Pia mkuu
huyo aliongeza kuwa shule hiyo ni jumba la kuandaa viongozi wazalendo na wenye
uchu nan nchi yao hasa katika kazi ya usimamizi wa rasilimali ya za nchi.
Amesema kuwa
msingi imara wa taifa la leo ni kuwajengea watoto elimu ya kujitengemea ili
pindi ambapo wanapohitimu elimu yao ya vyuo vikuu kutotegea kuajiriwa bali
wafikirie kuajiriwa zaidi.
Shule ya
Peace House kwa sasa ina jumla ya wananfunzi 344 ambapo wanafunzi 61 walihitimu
elimu ya kidato cha nne ambapo shule hiyo kwa sasa ni mcghanganyiko kwa
wanafunzi ambao ni yatima na wanaolipiwa
karo na wazazi wao.

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia