JKT OLJORO YALAZIMISHWA SARE YA BAO 2-2 NA COAST UNION YA TANGA
washabiki wa coast Union wakiwa wanacheza mara baada ya mechi kuisha katika uwanja wa kumbukumbu ya sheikh amri abeid jijini Arusha
Timu ya JKT OLjoro leo imeweza kulazimisha sare ya bao moja kwa moja katika uwanja wa nyumbani mara baada ya wapinzani wao Coast union ya tanga kujipanga vilivyo.
Coast Union iliweza kujiandikia bao la kwaza kupitia kwa mchezaji wake Kassim Seleman katika dakika ya 35 huku goli la pili likifungwa na Said swedi katika dakika ya 77 kwa upande wa magoli ya JKT Oljoro iliweza kujipatia bao la kwanza kupitia kwa mchezaji wake Paul Nonga katika dakika ya 50 huku bao la pili likifungwa na Meshack Nyambele katika dakika ya 50
Mchezo wa leo haukuwa na mashabiki wengi na hiii inatokana na washabiki wengi kujiandaa kwenda kuangalia mechi ya simba na yanga (watani wa jadi ) ambayo inachezwa leo usiku katika uwanja wa taifa

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia