WAKULIMA MILIONI MOJA WAPATIWA ELIMU YA KILIMO HIFADHI
Mkuu wa wilaya ya Arumeru , Nyerembe Munasa akiwa anafungua mkutano wa wadau wa kilimo leo katika hotel ya Naura spring jijini hapa
SHIRIKA la mtandao wa kilimo hifadhi Afrika(ACT)limefanikiwa kuwafikia na kuwapatia wakulima zaidi ya Milioni Moja elimu ya kilimo hifadhi huku kwa upande wa Tanzania wakulima zaidi ya Elfu thelahini nao wamepatiwa elimu ya kilimo hicho ili kuboresha zaidi Kilimo hicho.
SHIRIKA la mtandao wa kilimo hifadhi Afrika(ACT)limefanikiwa kuwafikia na kuwapatia wakulima zaidi ya Milioni Moja elimu ya kilimo hifadhi huku kwa upande wa Tanzania wakulima zaidi ya Elfu thelahini nao wamepatiwa elimu ya kilimo hicho ili kuboresha zaidi Kilimo hicho.
Hayo
yamesemwa na mkurugenzi wa shirika hilo
Mhandisi Said Mkwomwa wakati alipokuwa akiongea na wakulima mbalimbali wa kanda
za Afrika mashariki, Afrika ya kusini pamoja na Afrika ya kati.
Alisema
kuwa wakulima hao wamepatiwa elimu hiyo ili kuweza kufanya kilimo ambacho kina
tija zaidi tofauti na kilimo cha kawaida ambacho kimekuwa ni mzigo mkubwa sana kwa jamii.
‘ndani
ya nchi hizi zipo baadhi ambazo zimeshafanikiwa sana lakini kwa upande wa
Tanzania Kilimo hiki kipo ila hakijafanikiwa sana kutokana na wakulima wengi
sana kutegemea kilimo cha asili ambacho kinahusisha zaidi mifugo,kitu ambacho
kina haribu mazingira na wao wenyewe kuchoka sana sasa ni vema kama wakatumia
zaidi hiki kilimo cha kuhifadhi mazingira ambacho kina faida sana kwa wakulima mbalimbali”alisema Said
Alitaja
faida kubwa sana
ya kutumia aina kilimo hicho hapa nchini kuwa ni pamoja na kuhifadhi mazingira
hasa maji yaliopo ardhini, huku pia aina hiyo ya kilimo ikisaidia kupunguza na
kutatua changamoto mbalimbali za Mabadiliko ya Tabia za nchi ikiwemo ukame
ambao umekuwa ni chanzo cha njaa kwa jamii.
Awali
MKUU wa wilaya ya Arumeru , Nyerembe Munasa amewataka wakulima kuachana na
kilimo cha mazoea badala yake kutumia mfumo wa kilimo hifadhi
ambacho kimeonekana kuwa cha manufaa makubwa kwa wakulima wadogo barani
Afrika na ulimwenguni kwani kimekuwa kikikabiliana na mabadiliko ya tabia ya
nchi .
Nyerembe
alisisitiza kuwa, kilimo hicho kitawezesha kwa kiasi kikubwa sana kuongeza tija
katika uzalishaji wa mazao pamoja na kuondoa tatizo la njaa hususani katika
maeneo ya vijijini kwani wakulima wengi hawana elimu hiyo kwani wengi
wamekuwa wakitumia kilimo cha mazoea na kujikuta wakipata hasara kutokana na
mabadiliko ya hali ya hewa ambayo yamekuwa yakisababisha ukosefu wa mvua kwa
maeneo mengi.
Aidha
aliwashuri wakulima mbalimbali Afrika kujenga mtandao wa
kufahamiana na kubadilishana uzoefu juu ya kilimo hicho na kuwataka
wadau wa kilimo wajitokeza kusaidia maendeleo ya kilimo ili kukiwezesha
kilimo hicho kuenea maeneo mengi hapa nchini
Pia
alisema kuwa, kilimo hicho kinasaidia kuondoa wadudu waharibifu shambani
ikiwa ni pamoja na kuhifadhi mazingira na kumwezesha mkulima kuweza
kulima kilimo chenye tija na kuongeza ubora katika kilimo hicho na hatimaye kuongeza
hata mavuno

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia