TANZANIA IPO CHINI KATIKA UZAJI WA NGOZI NJE YA NCHI

Imebainika kuwa pamoja kuwa Tanzanina ni nchi ya tatu kwa kuwa na mifugo mingi duniani lakini ndio nchi ambayo ipo chini katika kuzalisha  la ngozi zenye ubora.

Hayo yamebainishwa jana na mkurugenzi wa taasisi ya teknolgia  ya ngozi ambayo makao makuu yake yako jijini Dar es salaam Pro.John Kondoro wakati alipokuwa akifungua mkutano wa siku sita wa wadau mbalimbali wanaozalisha ngozi hapa nchini pamoja na wananchi wa Somalia .

Alisema kuwa nchi yetu imekuwa ni nchi yenye mifugo mingi lakini ndio nchi ambayo inaingizia nchi kipato kidogo kuliko sekta zote zile.

Alibainisha kuwa nchi yetu imekuwa ikizalisha ngozi nyingi ambazo hazina ubora hali ambayo inafanya mpaka pato la ngozi ambalo linauzwa nje ya nchi kuwa dogo kutokana na ngozi zetu kutokuwa na sifa ambazo zinatakiwa.

“unajua unakuta ngozi  za wanyama wetu hazina ubora  kwani ngozi zingine mfugaji amepiga muhuri sehemu ambayo haikutakiwa kupigwa muhuri ,wakati mungine ngozi zinakuwa na ukurutu ambao labda unakuta ng’ombe yule au mfugo huyo aliugua na nyingine unakuta hajapewa chakula cha kutosha  hivyo  pia hupelekea ngozi zetu kutokuwa na ubora”alisema Pro.Kondoro

Kondoro alisema aliipongeza serekali yatu kwa kutengeneza sera ya kuboresha ngozi ambapo alisema kuwa katika sera ya ngozi ya mwaka 2007 inazungumzia maboresho ya ngozi ambapo wameweka asilimia ya ubora wa ngozi inayotakiwa kuuzwa nje ya nchi ambapo  awali ilikuwa ngozi inayounzwa nje ya nchi inatakiwa kuwa asilimia 40%na kupandisha hadi kufikia asilimia 90%  kwa ngozi ambazo zimechakatwa.

Kwa upande wake waandaaji wa semina hiyo Dr.Albert Mmari alisema kuwa semina hii inalenga kuwapa uzoefu wa namna ya shughuli za machinjio zinazofanywa ,namna ngozi zinavyoandaliwa na jinsi zinavyopimwa ubora ambapo alibainisha kuwa watatembelea kituo cha machinjio cha jijini Arusha (Arusha meet) kilichopo sakina.

Aliwataka wafugaji kutunza ngozi ikiwa ni pamoja na kuangalia sehemu ambazo wanapiga mihuri mifugo yao na kuwasisitiza wawapemifugo yao chakula cha kutosha ili kuweza kuboresha ngozi hizo.

Adha alisema kuwa iwapo vyote hivyo vitafanywa basi pato la taifa litaweza kuongezeka kupitia mifugo yetu ambapo aliongeza kuwa mkutano huu umeshirikisha wadau kutoka mikoa mbalimbali hapa nchi wakiwemo kutoka mikoa ya Kagera,Pwani,Mara,Musoma ,Arusha pamoja na wageni kutoka nchi ya Somalia.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia