
Mgombea udiwani akiwa anapanda gari la polisi
KATIKA
hali isiyokuwa ya kawaida mgombea Udiwani katika kata ya Daraja mbili
mkoani Arusha Prosper Msofe anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani
hapa kwa makosa ya kumshambulia Bw Rama Kalamba ambaye ni Mhamasishaji
mkuu wa kampeni za kusafisha jiji hasa kwa wafanyabaishara wadogo
wadogo “Machinga”
Akiongea
na libeneke la kaskazini, mjini hapa kamanda wa Polisi bw Liberatus Sabas alisema
kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili na nusu katika eneo
la france Kona ambapo mtuhumiwa huyo alimshambulia mhamasishaji wa Jiji
la Arusha na kusababisha madhara makubwa
Kamanda
Sabas aliongeza kuwa ndani ya eneo hilo mgombea huyo alikuta mhasishaji
wa Jiji akiwa katika shuguli zake za kawaida ambapo alikuwa anawatoa
wanawake ambao walikuwa wanauza bidhaa nje ya soko la muda la viwanja
vya Nmc na ndipo mgombea huyo alipohoji uhalali wa kuwatoa wanawake hao
katika eneo hilo
Alisema
kuwa mara baada ya kumuhoji mhasishaji huyo mtuhumiwa huyo alimfanyia
shambulio kwa kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake hali ambayo
ilisababisha Tafrani kubwa sana katika eneo hilo ambalo wafanyabaishara
walikuwa wanaendelea na biashara zao
‘baada
ya kuhoji alivunja sheria na kuanza kumsambulia kwa kumpiga haraka
haraka huyu mhasishaji ambaye yupo kwa mujibu wa sheria ya Jiji bila
kujua kuwa anavunja sheria ya Nchi na ndipo tulipopata taarifa juu ya
tukio hilo na kisha kufika na kumchukua mtuhumiwa huyo ambaye alikatiwa
RB namba AR/RB/12648/2012 ambapo kosa ni shambulio la kawaida katika
kituo cha polisi cha Kati”alisema
Awali
katibu wa Chadema kwa Wilaya ya Arusha Martin Sarungi alisema kuwa
pamoja na kuwa polisi walimshikilia Mgombea huyo lakini bado wamefanya
uonevu wa hali ya juu sana na hiyo ni mipango ya kumuondoa katika
uchaguzi wa kata ya daraja mbili.
Aliongeza
mahali ambapo wanapoona kuwa ni uonevu ni pale ambapo polisi
walimpeleka katika zahanati ya Polisi kwa ajili ya kutibiwa majeraha
mbalimbali ambayo walikuwa nayo lakini askari hao waliokuwa na silaha
kali za moto walimpeleka moja kwa moja hadi mahakama ya Maromboso ambapo
pia mshatakiwa wao hakuweza kusomewa mashitaka kutokana na kuwa na hali
mbaya ya kiafya hali ambayo iliwalazimu kumrudisha katika Hospitali ya
Mount Meru
“sasa
hapa unaona hawa polisi wanashirikiana na chama tawala na hizi ni mbinu
tu ila hata wafanyeje sisi bado ile ni kata yetu kwa sababu wewe huwezi
kumchukua mtu useme kuwa unampeleka zahanati kumbe unampeleka mahakamani
ukifika mahakamani chini ya ulinzi mkali unashindwa kusoma mashitaka
kutokana na kuzidiwa na kipigo unamchukua tena na kisha kumrudisha
hospitali ya mkoa chini ya uangalizi wa polisi je tueleweje kama sio
mbinu za kisia
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia