CHADEMA WACHACHAMAA KATIKA KAMPENI ZA UDIWANI ARUSHA

Kampeni za CHADEMA kuwania kiti cha Udiwani katika kata ya Daraja Mbili mkoani Arusha zilizinduliwa Jumamosi Oktoba 6 2012, huku Sakata la hivi karibuni la kutoroka kwa mahabusu chini ya ulinzi mkali wa askari polisi katika mahakama kuu ya kanda ya Arusha likichukuwa sura mpya na kutawala kampeni hizo.

Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki Kamanda mpambanaji Joshua Nassari maarufu kama (Dogo janja) akifungua kampeni hizo alionyeshwa kushangazwa kwa hatua hiyo huku akidai kuwa Serikali isipo chukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti (CHADEMA) Usa River basi ni wazi kuwa patachimbika na Nchi haitatawalika wala kukalika

akishangiliwa na umati mkubwa uliohudhuria  uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa udiwani katika kata ya daraja mbili alidai kuwa ni maigizo tu hayo yanayoendelea na CHADEMA hawapo tayari kuchezewa filamu hiyo kamwe

Kamanda Lema akihutubia umati mkubwa wa watu

Habari za ndani zinasema kuwa mahabusu hao waliotoroka wanatuhumiwa na mauaji ya aliyekuwa mwenyekiti wa chadema ambapo waliotoroka ni wawili huku wanne wakibakia magereza

Awali wakati akihutubia wananchi wa kata ya daraja mbili Nassari alisema kuwa kamwe hawatakaa kimya kutokana na filamu hiyo ya kutoroka kwa mahabusu hao

Lema akimnadi mgombea udiwani kata ya daraja mbili Prosper Msofe

Hata hivyo aliweka wazi kuwa katika kinyang’anyiro hicho cha udiwani wanauhakika wa kuibwaga vibaya CCM kwa madai kuwa Arusha ni kisima cha Mabadiliko

Katika hatua nyingine Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Kamanda Godbless Lema ametamba chadema kushinda katika uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Daraja mbili Mkoani Arusha sanjari na maeno mengine hapa Nchini

Kamanda Ephata Nanyaro Mh.Diwani kata ya Levolosi jijini Arusha akihutubia jukwaani

Wakati akimnadi mgombea Udiwani wa kata hiyo anayefahamika kwa jina la Prosper Msofe,Lema alisema kuwa wanauhakika na mgombea wao kupita kwa asilimia100% katika uchaguzi huo

“Eee Mwenyenzi Mungu tunashukuru tumeshinda katika uchaguzi huu wa daraja mbili Ameni”Lema alianza kwa sala

Emmanuel Zachariah maarufu kama baba boni akihutubia mara baada ya kuvua gamba na kuvaa gwanda

Lema alitoa tahadhari kwa baadhi ya watu waliomtumia sms kuwa mgombea huyo hakubaliki kutokana na yeye kumiliki gorofa na kudai kuwa chama cha chadema hakiamini katika umaskini na ndio sababu kubwa ya wao kupiga vita umaskini

“Tuanahitaji kila mtu hapa afanikiwe,,na umaskini sio uhadilifu na tunapiga vita umaskini usiku na mchana na hatuwezi kuwa na chama  kinachojisifia nyundo na jembe wakati watu wanalima kwa trekta huku wakimwagilia kwa maji ya chini”alisema Lema

Alibainisha kuwa umaskini unaendelea kuwakandamiza wananchi na leo hii umri wa kuishi mtanzania umeshuka kutoka miaka 70 hadi 45 kutokana na watu kuishi katika mazingira magumu na kuwataka wananchi wapige vita umaskini hata kwa kuuza figo zao

Pia katika hatua nyingine alimtaka mgombea udiwani kutumia umbo lake la ubaunsa kuhakikisha ndani ya halmashauri anatumia umbo lake kucheza na wezi huku akimuonya endapo ataota pembe kwa kukiuka taratibu za chama basi watamfuta kamati kuu na uchaguzi kurudiwa upya

“Chadema haipendwi ubaunsa,kitambi na kombati inapendwa kazi ya kupigania wanyonge na kama utaleta mauzauza basi tutakupiga chini kama ilivyokuwa kwa Bayo,Mala na wenzake”alisema kamanda Lema

Kutokana na hilo umati mkubwa wa wafuasi hao ulishangilia kwa sauti ya juu huku wakimpongeza Lema kwa ushujaa wake huku wakipiga pipoooz power ndani ya viwanja hivyo vya shule ya daraja mbili Mkoani Arusha

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia