TANAPA WAZINDUA TUZO KWA MAALUM KWA AJILI YA WAANDISHI WA HABARI HAPA NCHINI

Meneja mahusiano wa shirika la Hifadhi ya Taifa(TANAPA)Pascal Shelutete akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania(TANAPA)limezindua tuzo maalumu kwa waandishi wa habari hapa Nchini ijulikanayo kama(TANAPA Media Awards 2012)katika maeneo ya uhifadhi pamoja na Utalii wa ndani lengo ikiwa nikuongeza uelewa juu ya wananchi kuhifadhi maeno ya hifadhi

Meneja mahusiano wa shirika hilo Pascal Shelutete katika uzinduzi huo  alisema kuwa kwa mwaka huu wa 2012 watatoa tuzo kwa waandishi wa habari watakao kuwa wameandika habari zitakazo saidia kuongeza uelewa kwa wananchi juu ya kuhifadhi wa maeneo yaliyotengwa kama hifadhi za taifa

Alisema kuwa wanahabari watakao jitoa kwa dhati kwa kuandaa vipindi,makala maalum zinazohamasisha juu ya utunzwaji wa maeneo ya hifadhi za taifa watatambua mchango wao kwa kutoa tuzo kama njia ya kuhamasisha waendelee kuwaelimisha Watanzania,hususani wanaoishi jirani na hifadhi hizo kwa kutambua umuhimu wa maeneo hayo

“Wanaishi jirani na hifadhi hizo watapata uelewa mkubwa wa kuacha kuvamia maeneo ya hifadhi,kuingiza mifugo ndani ya hifadhi,,kwa sababu ushirikianio baina ya shirika na  wananchi hao ndio utakao saidia kuhakikisha hifadhi hizo zinaendelea kudumu”alisema Shelutete

Aliongeza kuwa katika eneo la pili ambalo ni utalii wa ndani unaonyesha kuwa muamko wa watanzania kutembelea maeneo hayo ya hifadhi umekuwa ni wa chini sana huku akidai kuwa pengine ni jamii kutotambua maeneo hayo ya hifadhi pamoja na utamaduni uliojengeka kuwa wanaotakiwa kutembelea hifadhi hizo ni wageni kutoka nje tu

Alibainisha kuwa Mtanzania anawajibu wa kutembelea hifadhi hizo kwa kuona rasilimali zilizopo katika maeneo mbalimbali ya Tanznia

Aidha alisema kuwa vipindi hivyo pamoja na makala hizo zitakazo andaliwa na wanahabari hapa nchini ziwe za kuibua au kuanisha vivutio vilivyopo katika maeneo yaliyotengwa kama hifadhi za taifa pamoja na kuhamasisha watanzania kuona umuhimu wa kutembelea vivutio hivyo

Katika shindano hilo kutakuwepo na vipengele vitatu ambavyo ni Redio,Televisheni na Magazeti ambapo katika eneo hilo atapatikana mshindi wa kwanza hadi wa tatu hivyo kufanya washindi kwa ujumla kuwa kumi na nane

Washindi katika mchakato huo mshindi wa tatu katika kila eneo atajinyakulia pesa tasilimu shilingi500,000 pamoja na cheti huku wa pili akipata sh.shilingi 1,000,000 na cheti pamoja na ngao,mshindi wa kwanza ataibuka na kitita ta shilingi 1,500,000  ,cheti,ngao pamoja na safari ya kujifunza maswala ya utalii ya uhifadhi katika nchi za SADC

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia