PPF YATAKIWA KUFANYA UTAFITI KUPATA WANACHAMA WAPYA


Uongozi wa mfuko wa jamii wa pensheni( PPF)  na mifuko mingine hapa nchini imepatiwa changamoto ya kuhakikisha kuwa wanafanya utafiti wa kina ili kubaini fursa ya kupata wananchama wapya kutoka katika sekta isiyo rasmi.

Mgani rasmi Bi.Saad Mkuya akimkabidhi zawadi mshindi katika mkutano huu

Akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa 22 wa mwaka wa wananchama wa mfuko wa pesheni wa (PPF) na wadau wengine wa hifadhi ya jamii jana jijini Arusha Naibu Waziri wa Fedha Bi.Saada Mkuya Saalum alisema kuwa ni vyema mifuko hiyo ikafanya utafiti ili kubainin njia madhubuti za kuongeza wananchama hao wapya.

Bi.Mkuya alisema kuwa sekta isiyo rasmi imekuwa ikikua kwa kasi kubwa na hivyo kuajiri watu wengi hivyo ni vyema kutumia matokeo ya utafiti zitakazofanyika na kuchukua hatua zinazostahili za kuhakikisha wananchama waliopo katika sekta hiyo isiyo rasmi nao wanajiunga na kuchangia mifuko hiyo.

“Naomba nitoe rai yangu kwenu Uongozi wa mfuko wa PPF  na wengine mfanye utafiti ili kubaini njia  mbadala za kupata wananchama wapya katika sekta isiyo rasmi kwa kuwa inakuwa kwa kasi hivyo mkiwapata hawa kupitia utafiti wenu kitawasaidia kupata michango na idadi ya wananchama itabadilika.”alisema Bi.Mkuya

Aidha alisisitiza kuwa maazimio ya mkuatabno huo yawe dira katika kutekeleza majukum ya kuhakikisha kuwa mifuko ya hifaddhi ya jamii nchini ionakuwa kichocheo cha maendeleoya jamii na uchumi wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa mfuko wa PPF bw.Willium Urio alisema kuwa ifuko ya hifadhi ya jamii ni kichocheo cha uchumiwa nchi kutokana na uwekezaji ambao unafanywa na mifuko hiyo ikiwa ni pamoja na huduma nyingine mbalimbali za kijamii.

Bw.Williuma alisema kuwa mkutano huo utaambatana na uopimaji wa hiari wa magonjwa mbalimbali kama vile kisukari,virusi vya ugonjwa wa ukimwi,shinikizo la damu na uzito.

Pia alionngeza kuwa wananchama wa mfuko huo watapata fursa ya kutembelea mojawapo ya mbuga za wanyama hapa nchini “Tarangire”ili kujionea mambo mbaklimbali yaliyopo katika mbuga hiyo ikiwa ni kuhimiza utalii wa ndani.

Naye mwenyekiti wa bodi wa mfuko huo Dkt.Adolf Faustine Mkenda  alisema kuwa kiwango kimekuwa kikiongezeka ambapo  mfuko umeendelea na uwekezaji katika vitega uchumi mbalimbali ambapo jumla y sh.bilioni 837.6 ziliwekezwa kufikia mwishoni mwa mwaka 2011 ukilinganisha na shilingi 672.2 bilioni  mwishoni mwa mwaka 2010.

Hata hivyo alifafanua kuwa mapato ya yatokanayo na uwekezaji yalipanda kwa asilimia 110 kutoka shilingi 43.45 bil. Zilizopatikana katika mwaka 2010 hadi kufikia jumla ya  sh.91.38 bil. Zilizopatikana mwaka 2011 katika kipindi hicho cha January hadi Juni mwaka 2012 mapato yatokanayo na uwekezaji yamefikia jumla ya sh.47.714  bilioni kati ya lengo la sh.47.71 bil. Kwa kipindi hicho.

Mkutano huo unaendelea katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa (AICC) uliopo jijini Arusha uanatarajiwa kumalizika rasmi tarehe 13 october ambapo pia umeshirikisha  wadau wa mifuko ya hifadhi kutoka nchi ya Zambia,Burundi,Rwanda na Afrika Kusini na wenyeji Tanzania.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia