SHULE YA MSINGI CHEMKAYAPATIWA MSAADA
Shule ya Msingi ya Chemka iliyopo nje kidogo wa mji
wa Bomang’ombe wilayani Hai imepokea majengo yaliyojengwa na Bibi Kizee wa
Kijerumani Elisabeth Dorr(89) kupitia shirika la Ako lililoko mjini Moshi.
Shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Chemka ilipata
ufadhili huo mwaka 2008 kupitia kanisa katoliki parokia ya Chekereni kupitia
shirika la AKO-Moshi
Majengo hayo ni pamoja na madarasa matatu,nyumba
mbili za walimu,bwalo la chakula,stoo na ofisi ya shule pamoja na kugharamia
uunganishaji wa umeme na kuvuta maji ya bomba ambapo Bibi Dorr alitoa jumla ya
Euro 50,000 ambazo ni sawa na shilingi 93,554,698.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo,David Mosha ameeleza kuwa
Bibi huyo wa Kijerumani pia akatika fedha hizo alitoa madawati 66,meza 4,viti
4,makabati 7 ya ukutani,sufuria mbili kubwa,beata stoves 2,meza na mbenchi 15 kwa
ajili ya matumizi ya bwalo
Mosha ameeleza kuwa awali Bibi huyo alijenga darasa
moja mwaka 2008 na baadaye mwaka uliofuata alimtuma mwenyekiti wa Shirika la
AKO-Tanzania,Klaus Boehme na kufurahishwa na usimamizi wa miradi hiyo shuleni
hapo.
Akipokea rasmi miradi hiyo,Mkuu wa wilaya ya Hai
Novatus Makunga amewataka wakazi wa kijiji cha Chemka kuyatunza majengo hayo
kwa nguvu zao zote na pia kuhakikisha wanaingia katika kampeni ya kupanda miti
kutokana na eneo hilo kunyemelewa na jangwa kutokana na kuwa na idadi kubwa ya
mifugo
Aidha Makunga amewataka kutumia fursa ya vyumba bora
na vizuri pamoja na umeme kuchangia ununuzi wa kompyuta kwa ajili ya kuanzisha
darasa la kompyuta pamoja na kurahisisha kazi za utawala.
Aliahidi kuchangia kompyuta moja kwa ajili ya
kuanzia na kuongeza kuwa siyo kwamba kukiamilika kwa majengo hayo kutaifanya
shule hiyo kufanana na shule za mjini lakini pia kutawaingia katika mazingira
ya kisasa ya teknolojia zinazotumika katika maeneo ya mjini



0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia