ZAIDI YA MILIONI TANO ZAPATIKANA KWENYE HARAMBEE YA NYUMBA YA KUISHI ASKAI POLISI MANYARA
MKUU wa Mkoa wa Manyara,Elaston Mbwilo
ameongoza harambe na kupatikana shilingi 5,050,000 (milioni tano na elfu
hamsini) kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za kuishi askari wa kituo cha polisi cha
kata ya Naisinyai wilayani Simanjiro.
Mbwilo ambaye alichangia shilingi milioni moja
alianzisha harambee hiyo ili nyumba hizo za askari wa kituo hicho kipya cha
Polisi kata ya Naisinyai zijengwe na waweze kuishi kwani zitawapunguzia askari
hao kero ya makazi.
Aliagiza wananchi,viongozi wa kijij na kata ya
Naisinyai wakishirikiana na kampuni ya TanzaniteOne kuhakikisha kuwa wanamaliza
ujenzi wa nyumba hizo kabla ya mwezi Desemba ili aweze kuzindua rami kituo
hicho.
“Nikizindua leo kituo hiki bila kuwa na nyumba
za kuishi askari wetu hata ninyi mtanishitaki hivyo nawachangia sh milioni moja
na muongeze nguvu mkishirikana na TanzaniteOne ili mjenge nyumba hizo nije
nizindue,” alisema Mbwilo.
Kwa upande wake,Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya
TanzaniteOne Dotto Medard alisema kituo hicho kimejengwa na wananchi hadi
kwenye lenta nao wakamaliza kwa kupaua kuweka umeme,maji na kununua samani za
ofisi.
Medard alisema awali kituo hicho kiliwekwa
jiwe la msingi na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema na hadi
kukamilika kwake kampuni ya TanzaniteOne imetumia gharama ya shilingi milioni
60 kukimalizia.
Naye,Diwani wa kata ya Naisinyai,Kilempu
Kinoka ambaye alichangia shilingi laki tano kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo
za askari polisi wa kituo hicho alimuhakikishia mkuu huyo wa wilaya kuwa
watajenga nyumba hizo.
“Kwa nafasi ya pekee mkuu wa mkoa hili
tutalitekeleza kwani kata ya Naisinyai inaongoza hapa nchini kwa ulinzi
shirikishi na polisi jamii kwa hiyo hili litafanyika kwa juhudi kubwa na moyo
thabiti,” alisema Kinoka.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya TanzaniteOne,Weseel
Marias alisema kampuni yake na jamii ya eneo hilo watajipanga kikamilifu
kuhakikisha kuwa agizo hilo la mkuu wa mkoa linatekelezwa ili azindue kituo cha
polisi na nyumba za askari.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia