ARSENAL YAMUWEKA ZAHA KATIKA RADA ZAKE, KWA AJILI YA NAFASI YA THEO WALCOTT



Klabu ya Arsenal iko katika mchakato wa kutafuta mchezaji atakayeziba pengo la THEO WALCOTT baada ya kuingia katika kinyang’anyiro cha kutafuta saini ya mchezaji wa Crystal Palace WILFRIED ZAHA. Aliyekuwa meneja msaidizi wa Arsenal PAT RICE ambaye bado anafanya kazi na klabu hiyo pamoja na kustaafu katika majira ya kiangazi alikuwa akimfuatilia mchezaji mwenye umri wa miaka 19 katika mchezo ambao timu hiyo ilishinda kwa mabao 4-3 dhidi ya Barnley Jumamosi. Arsenal katika kipindi cha karibuni imekuwa ikituma wapelelezi wake katika michezo ya Palace mahsusi kwa ajili ya kufuatilia kiwango cha Zaha hivyo kuwepo uwezekano mkubwa wa kumyakuwa kinda huyo. ZAHA ambaye thamani yake inafikia kiasi cha paundi milioni 12 anaweza kuwa mchezaji mpya kujiunga na Arsenal kutokea katika ligi za chini kama klabu hiyo ikishindwa kumsainisha WALCOTT mkataba mpya. WALCOTT ambaye mkataba wake umebakia miezi isiyopungua 12 amekataa kusaini mkataba mpya ambao utakuwezesha kulipwa kiasi cha paundi 75,000 kwa wiki ingawa bado wapo katika mazungumzo zaidi kupata muafaka wa sakata hilo.

SUDAN YANYANG'ANYWA ALAMA NA FIFA.
Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA limeinyang’anya ushindi wa mabao 2-0 Sudani iliyopata dhidi ya Zambia katika mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 kwasababu mmoja wa wachezaji aliyefunga mabao hayo hakuruhusiwa kucheza. Kamati ya nidhamu ya FIFA ilifafanua katika taarifa yake kuwa mchezaji huyo aitwaye SAIF ALI hakuruhusiwa kucheza katika mchezo huo uliochezwa June 2 mwaka huu jijini Khartoum. Zambia walilalamika kuwa ALI alicheza katika mchezo huo pamoja na kuwa na kadi mbili za njano katika michezo miwili tofauti ukiwemo mchezo ambao Zambia iliifunga Sudan katika mchezo wa robo fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika uliochezwa Februari mwaka huu. FIFA ilikubaliana na malalamiko hayo ya Zambia baada ya kufanya uchunguzi na kuipa ushindi wa mabao 3-0 na pointi tatu nchi hiyo huku ikilitoza faini Shirikisho la Soka la Sudan ya dola 6,430. Zambia sasa inaongoza katika kundi D ikiwa na alama sita katika michezo miwili waliyocheza na Sudan imedondoka mpaka nafasi ya tatu ikiwa na alama moja, Ghana wako nafasi ya pili wakiwa na alama tatu na Lesotho ni ya mwisho wakiwa na alama moja.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia