MREMBO WA UTALII MANYARA KUPATIKANA OCTOBA 12
WANYANGE 14 wanatarajiwa kuchuana kwenye
mashindano ya kumtafuta Miss Utalii wa Mkoa wa Manyara unaotaraji kufanyika
Octoba 12 mwaka huu kwenye ukumbi wa Kangaroo Hoteli Mji mdogo wa Mirerani
Wilayani Simanjiro.
Akizungumza jana na waandishi wa habari,Mratibu
wa michuano hiyo Mosses Komba alisema maandalizi ya mpambano huo
yameshakamilika na hivi sasa warembo hao wanafanya mazoezi kila siku kwa
kupanda milima ya madini ya Tanzanite.
Komba alisema kupitia kampuni yake ya New
Vision mashindano hayo yanatasindikizwa na mwanamuziki maarufu Wanne Star
anayefanya muziki wake kwa kuimba na kucheza nyimbo za asili,Morgan Sound Band
na Sarakasi.
Alisema michuano hiyo ya Miss Utalii mkoa wa
Manyara inadhaminiwa na kampuni ya Ken Family General Trading Co,Radio 5,Kangaroo
Hotel,Manga Gems,White Fashion,Manyara Inn na Baba G Intertainment.
Alisema warembo watakaoshikiri mashindano hayo
ni wasichana wa wilaya zote tano za mkoa huo ikiwemo
Simanjiro,Kiteto,Mbulu,Hanang’ na Babati ambao ni wanyange wa
kiiraq,kimasai,kibarbaig na kifyomi.
Alitoa wito kwa watu wote wanaopendelea
burudani za urembo kujitokeza kwa wingi kwenye mashindano hayo ili kuwaunga
mkono wasichana hao wa mkoa wa Manyara ambao wote ni chipukizi katika masuala
ya urembo.
“Lengo la mashindano hayo ni kuutangaza utalii
wa ndani wa mkoa wa Manyara na ninawapongeza wazazi wa wasichana hawa wa mkoa
wa Manyara kwa kuruhusu watoto wao wa kike kushiriki mashindano hayo,” alisema
Komba.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia