IMEBAINIKA kwamba Ugonjwa wa Saratani ya Ini inasababishwa na vijidudu ninavyo kula Mahindi na Karanga Mashambani.
Vimelea vya vijidudu hivyo maarufu kama Aflatoxin ndiyo chanzo kikubwa cha ugonjwa wa Saratani ya Ini,unaosumbua Watanzania.
| Ugonjwa wa Aflatoxin unaoshambulia mahindi na karanga, ambayo pia ndiyo chanzo kikubwa cha Saratani ya Ini |
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Mkutano wa Kilimo kwa nchi
za Afrika Mashariki na Kati unaonedelea hivi sasa katika Hoteli ya
Ngurutodo jijini Arusha, Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii Dk Seif Rashid alisema, kwamba Watanzania wengi wanasumbuliwa na
ugonjwa wa Saratani ya Ini kutokana na uchafu wa mazao na vyakula
wanavyokula.
“Ugonjwa wa Saratani ya Ini inatokana na vimelea vya vijidudu vya
Aflatoxin,vijidudu hivyo vinapatikana katika mahindi na karanga na
chanzo chake kikuu ni maeneo yenye uchevuchevu”alisema Naibu Waziri huyo
na kuongeza:
“Ili watanzania waepukaane na ugonjwa huu, wanapswa kuzingatia
utunzaji wa vyakula vyao kuanzia mashambani hadi katika uandaaji wa unga
wa ugali na uji”.
Akichangia mada katika Mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa uzalishaji
katika idara za kijamii Jesca Eriyo alisema kwamba, suala la utunzaji wa
chakula inapaswa kuanzia katika ngazi ya familia.
“Kila mwanafamilia anapswa kutunza mazao katika hali ya usafi ili
kuepukana na maradhi yanayosababishwa na vijidudu vinavyosababisha
magonjwa ya chakula ambayo pia ni hatari kwa afya za watumiaji”alisema
Eriyo.
Katika hatua nyingine alisema kwamba, haina maana kutunza chakula ama
mazao katika hali ya usafi wakati mifugo inaachwa ikizagaa ovyo kwani
ukiepukana na uongjwa wa aflatoxin katika mazao utakutana nao katika
mazao ya mifugo kama nyama,maziwa na mayai.

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia