Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam
VURUGU za waumini wa Dini ya Kislam na Wakristo zilizozuka leo katika
eneo la Mbagala Majimatitu jijini Dar Es Salaam zimesababisha Makanisa
matatu kuchomwa moto.
Vurugu hizo zilizotokana na utani wa watoto wadogo wenye umri wa
miaka 12 zimesababisha waumini wa Dini ya Kislamu kuchoma makanisa hayo.
Utani wa watoto hao ulitokana na mtoto wa Kislamu kumwambia mtoto wa Kikristo kwamba kitabu chao wanachokiamini cha (Quran) kina nguvu kushinda kitabu cha Kikriston (Biblia) na kwamba ukikikojolea kitabu hicho unakuwa mwendawazimu (chizi,kicha).
Utani wa watoto hao ulitokana na mtoto wa Kislamu kumwambia mtoto wa Kikristo kwamba kitabu chao wanachokiamini cha (Quran) kina nguvu kushinda kitabu cha Kikriston (Biblia) na kwamba ukikikojolea kitabu hicho unakuwa mwendawazimu (chizi,kicha).
Mashuhuda wa tukio hilo waliiambia tovuti hii ya Habarimpya kwamba
baada ya watoto hao kubishana juu ya nguvu za Quran mtoto mwenye imani
ya Dini ya Kikristo aliamua kukojolea kitabu hicho alichokuwa nacho
mwenzake ili abaini kama kweli atakuwa chizi na baad ya hapo akamwambia
mwenzake kuwa mbona hajawa chizi.
Watu wakikimbia baada ya Askari Polisi kutawanya umati huo kwa mabomu ya machozi
Ramadhani Omaary Juma ambaye ni muuza matunda katika eneo hilo
akizungumza na tovuti hii ya Habarimpya katika eneo hilo alisema kwamba,
baada ya utani huo mtoto mwenye imani ya Dini ya Kislam alikimbia
Msikitini na kuita wenzake kuwa kuna mtoto wa Kikristo amekojolea kitabu
chao kitakatifu.
“Kwakweli haya yaliyotokea ni yakushangaza sana haiingii akilia kama
utani wa watoto unaweza kuleta vurugu kiasi cha Makanisa kuchomwa moto
na vita kubwa kuzuka katika eneo hilo na muda wowote mauaji yanaweza
kutokea,haya yote yanatokana maamuzi ya ajabu watu hawa walipaswa
kuuliza chanzo cha tukio hilo kwanza alisema Juma”.
Naye Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Salaam Suleimani Kova
amesema kwamba Askari wa Jeshi la Polisi tayari wameweka kambi katika
eneo hilo na kazi ya kutuliza vurugu hizo imeanza kufanikiwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Sadick Meck Sadick
alisema kwamba Serikali ikomakini katika suala hilo na kwamba hali ya
utulivu itarudi katika maeneo hayo.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia