MWANAMKE ACHOMWA MOTO KISA WIVU WA MAPENZI


MWANAUME mmoja nchini Nigeria anashikiliwa na polisi baada ya kummwagia petroli na kisha kumchoma moto aliyekuwa mkewe kutokana na wivu wa mapenzi.
Kehinde Adesamuye, 39, mkazi wa Lagos nchini Nigeria anadaiwa kumchoma kwa moto wa petroli aliyekuwa mkewe Janet Udegba, 35 katika mitaa ya Ikotun baada ya kuwa na hasira kutokana na kuhisi kuwa mkewe huyo ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamume
mwingine.
Janet alisema wakati wa tukio hilo alikuwa katika eneo lake la biashara akiuza vyakula kabla ya Kehinde kufika hapo usiku huo na kumwagia petroli maeneo ya
mgongoni na kumwasha kwa kutumia njiti ya kibiriti.
Hata hivyo alisema Wanigeria hawatamwachia huru Kehinde kutokana na kile alichokifanya kwake. Akisimulia mgogoro wao anasema;
"Mume wangu amekuwa na wivu daima. Amekuwa na tabia ya kunipiga kila wakati pasipo kuomba msamaha. Nimejaribu mara nyingi kuachana naye lakini yeye daima ananitisha kuwa lazima atanidhuru. Niliendelea kuishi na yeye kwa kuwa nilikuwa na hofu na maisha yangu, aliwahi kuniambia kuwa sitaweza kutoroka
hata siku moja.
"Mwezi uliopita nilimweleza kuwa nitaondoka na kwenda nje ya jiji la Lagos, aliniruhusu na kudai kuwa hana tatizo na mimi ila aliniambia kuwa atanifanyia jambo
moja ambalo sitakaa nikasahau, unaona alichonifanyia. Alitaka kuniua."
"Nimekuwa nikifanya kazi ya kuuza vyakula katika eneo la kuzunguka Ikotun. Kuna wanawake na wanaume pia wanaofanya biashara hii. Sisi wote kwa pamoja ni kama marafiki wa kawaida tu.
"Mwishoni mwa wiki iliyopita mmoja kati ya wafanyabiashara wenzangu alikuwa na sherehe ya mtoto wake, tulikwenda katika sherehe ile tukiwa pamoja. Kehinde alikuwa huko pamoja nami, mmoja kati ya wafanyabiashara wenzangu alinipa kinywaji, niliichukua kwa kuwa nilikuwa katika unywaji pia."
Anasimulia Janet "hiyo ndiyo ulikumwa mwanzo wa tatizo, akasema kuwa nilimbusu mtu mwingine mbele ya uwepo wake. Alisema kuwa nilikunywa pombe ambayo mwanamume mwingine alikunywa. Tangu hapo alianza kunipa onyo kwamba atakabiliana na mimi pindi tutakapofika nyumbani.
Janet anasema ili kuwa upande salama aliamua kumwita mdogo wake na kumwambia kuwa aje kulala nyumbani mwake kwa usiku huo.Mimi sikutaka kupigwa na mume wangu nilijaribu kumwelewesha lakini hakuelewa.
"Baada ya kufika nyumbani alianza kunilaani na kunitesa huku akiongea kila aina ya neno mbele ya mdogo wangu. Lakini sikuweza kumjibu wala kuongea lolote kwa kuwa sikutaka kugombana na yeye. Tabia hii iliendelea hadi Jumamosi. Alinipiga hadi mateke kutoka kitandani lakini mimi nililala juu ya sakafu.
"Nilipoamka siku ya Jumapili, alikuwa amekwenda nje. Niliingia bafuni na kuoga haraka kwa kuwa sikuhitaji anikute akirudi. Lakini aliniwahi, na kuanza kunipiga bila sababu ya msingi. Alinipiga sana mpaka nikafikiria kuwa siku hiyo ataniua kabisa. Aliniacha baada ya baba mwenye nyumba kuingilia kati ugomvi ule. Baada ya
kipigo kile niliondoka mpaka kwa mdogo wangu." alisema Janet.
"Serikali lazima ihakikishe kuwa Kehinde analipa kwa kile alichonifanyia mimi. Mimi ni yatima. Sina mama, sina baba. Ninauza biashara ya vyakula ili niishi. Sasa nimetumia pesa zangu zote kwa ajili ya matibabu. Kwa kweli kwa sasa nahitaji msaada." alisema.
Akisimulia zaidi anasema baada ya kwenda kuishi kwa mdogo wake aliendelea na shughuli zake, lakini Kehinde aliendelea kumfuata na kumtaka amsamehe kutokana na kipigo alichompa.
Kehinde alijaribu kutuma rafiki zake ili wamwombee msahama kwa Janet lakini alikataa jambo lililopelekea Kehinde kumvizia akiwa katika biashara zake na kumwagia petroli kisha kumchoma moto na kumsababishia majeraha kadhaa nyuma ya mgongo wake mpaka
miguuni. Mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi kwa ajili ya kujibu mashtaka yanayomkabili.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia